Home African Music Emmanuel Mgogo – Napenda Niwe Na Wewe

Emmanuel Mgogo – Napenda Niwe Na Wewe

Napenda Niwe Na Wewe by Emmanuel Mgogo MP3 MUSIC VIDEO

Napenda Niwe Na Wewe LYRCIS by Emmanuel Mgogo:
Mimi napenda niwe karibu na wewe
Bwana niwe na wewe
Univute niwe karibu na wewe
Bwana mimi napendaga

Maana hapa nilipo
Nipo moyoni na kiu zaidi
Nina kiu na wewe, kuwa karibu na wewe
Napenda ooh, ninapendaga

Nina haja na wewe bwana
Natamani ukae nami
Sioni mwingine bwana
Sijapata mwingine

Ila ni wewe wa kunifaa mimi
Wa kunitunza ila ni wewe
Tabibu wa karibu bwana

Usinipite pembeni bwana
Sina mwingine wa kunihurumia
Pale ninapo jeruhiwa
Na wanyang’anyi uwe karibu

We ni msamaria mwema utanihudumia
Utanifunga majeraha na kunifariji
Unionyeshe pendo lako
Maana wanipenda

Unionyeshe pendo lako
Maana wanipenda

Sioni la kunifurahisha
Nikiwa mbali na uwepo wako
Kama mti unang’olewa udongoni
Nitasinya na kudhoofika

Ninaomba univute niwe karibu nawe
Kama mti uliopandwa kando kando ya maji
Uzao wa matunda mazuri
Wala majani yake hayanyauki

Kila nitendalo nifanikiwe
Bwana naomba

Wewe ni maji ya uzima
Wewe ni maji yaliyo hai
Kisima cha uzima
Na upendo

Kama hayana na porini
Ayatamanivyo maji
Ndivyo nafsi yangu yakutamani wewe
Fanya hima usichelewe

Univute karibu nawe
Niwe na wewe

Mimi napenda niwe karibu na wewe
Bwana niwe na wewe
Univute niwe karibu na wewe
Bwana mimi napendaga

Maana hapa nilipo
Sijaridhika nina kiu zaidi
Nina kiu na wewe, kuwa karibu na wewe
Oooh ninapendaga

Kukaa na wewe
Ni shauku pekee
Ya moyo wangu bwana aah
Hapa nilipo sijaridhika

Natamani nipandishwe juu
Univute karibu na wewe
Karibu zaidi ya jana
Uwe nuru uniangazie

Pendo lako kama maji
Nizame kwenye kisima
Cha uwepo wako

Nimesoma katika neno lako Zaburi
Umesema ooh
Aketiye mahali pake pa siri
Palipo juu

Huyo atakaa katika uvuli wake mwenyezi
Ataokolewa na mitego ya adui
Silaha zote na mishale
Haitofanikiwa

Silaha zote na mishale
Haitofanikiwa

Nichue uniweke hapo bwana
Hili ni ombi la moyo wangu
Niketishe kwenye uwepo wako
Tuketishe kwenye uwepo wako

Usiniache gizani bwana
Peke yangu siwezi
Kaa nami, karibu nami
Ndani yangu nami ndani yako

Univute karibu nawe
Mikononi mwako niwe salama
Univute karibu nawe
Niwe na wewe bwana

Mimi napenda niwe karibu na wewe
Bwana niwe na wewe
Univute niwe karibu na wewe
Bwana mimi napendaga

Mimi napenda niwe karibu na wewe
Bwana niwe na wewe
Univute niwe karibu na wewe
Bwana mimi napendaga

Maana hapa nilipo
Nipo moyoni na kiu zaidi
Nina kiu na wewe, kuwa karibu na wewe
Napenda ooh, ninapendaga

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here